Viongozi waliotuma salamu Za rambirambi Kwa Hayati Benjamin William Mkapa




1595597598012.png

WANANCHI WASIMAMA BARABARANI KUAGA MWILI WA RAIS MKAPA

Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam, wameonekana wakisimama barabara kuonyesha heshima kwa mwili wa Rais Mkapa unaopelekwa katika Uwanja wa Uhuru kuagwa rasmi

Wananchi wa imani tofauti tofauti wamekuwa kando ya barabara wakipunga mikono na wengine wakimwaga maua ya kwa heri kwa Rais aliyetangulia mbele za haki

MWILI WA RAIS MSTAAFU MKAPA KUAGWA UWANJA WA TAIFA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa msibani nyumbani kwa marehemu, Masaki-Dar amesema Mwili wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, utaagwa kwenye uwanja wa Taifa Dar

Hata hivyo, amesema siku ya kuaga mwili huo itatangazwa baada ya taratibu zote kukamilika na taarifa kamili itatolewa baadaye


Updates
RAIS KIKWETE: NILIMJULIA HALI RAIS MKAPA JANA NA HALI YAKE HAIKUWA YA KUTIA SHAKA

Rais wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema hali ya kiafya ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa haikuwa mbaya alipoenda kumuona jana jioni hospitali

Amesema, “Jana jioni nilikwenda kumuona hospitali. Tulizungumza sana kwa karibu saa moja. Alikuwa na maumivu ila si yale maumivu ya kutoka kumuona mgonjwa na kumwambia mwenzako nimemuona mgonjwa ila eenhe!”

Ameongeza, “Nilipopata taarifa usiku wa manane kwamba Mzee amefariki niliuliza kumetokea nini tena kwasababu hakuwa mgonjwa wa kutia shaka na niliondoka nikamuaga kwamba nitakuja kukuona kesho ila siombei uendelee kukaa nyumbani, tuonane nyumbani”

Amemalizia “Kifo ni siri ya Mwenyezi Mkungu. Ila kubwa ni kwamba tumepoteza moja ya viongozi mashuhuri, Mkuu wa nchi yetu aliyetumikia taifa letu vizuri kwa uadilifu mkubwa na moyo wa upendo. Nawaomba Watanzani kuwa na moyo wa ustahimilivu na uvumilivu”

1595598580579.png

Rais Kikwete akisaini kitabu cha rambirambi msibani

Updates
TAARIFA ZAIDI KUHUSU MSIBA WA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa pole kwa Watanzania kwa kuondokewa na Rais Mstaafu wa awamu ya 3. Ameungana na Rais Magufuli kuomboleza na kama ambavyo amewasihi Watanzania kuendelea kuwa watulivu

Nimewaita kwa lengo la kuwapa ratiba nzima ya tukio hili hadi siku ya mazishi. Rais wetu pamoja na Kamati ya mazishi ya Kitaifa imeandaa utaratibu mzima wa tukio hilo ambapo Marehemu atazikwa Kijijini kwake Lupaso, Masasi Mkoani Mtwara

Lupaso ni Kijiji kilichopo pembezoni mwa Mji wa Masasi, si mbali sana. Mazishi haya yatafanyika Julai 29, 2020 siku ya Jumatano ya wiki ijayo - Kuanzia sasa tunaendelea kupokea waombolezaji pale nyumbani kwa marehemu

Tutatoa fursa kwa Watanzania wote Jumapili kwa shughuli za kuaga zitakazofanyika uwanja wa Taifa yaani Uwanja wa Uhuru, Dar. Shughuli za kuaga zitafanyika kwa siku 3 mfululizo, kuanzia Julai 26 hadi Julai 28 (Jumapili hadi Jumanne)

Jumapili kuanzia saa 4, dhehebu la Roman Catholic litaongoza Misa ambapo Watanzania watapata fursa ya kuanza kuaga mwili baada ya misa. Zoezi la kuaga litaendelea siku nzima hata kama ni usiku bado kutakuwa na fursa ya kuendelea kuaga mwili

Niwakaribishe pia watu wote hata Watumishi kwasababu shughuli hiyo tutaenda nayo hadi saa 6 mchana na baadaye Watumishi watarudi maeneo ya kazi. Shughuli za kuaga zitaendelea hadi saa 8 mchana. Baada ya hapo mwili utapelekwa Lupaso, Mtwara

Jumatano WanaLupaso, WanaMasasi, ndugu na jamaa na wote watakaofika kuanzia asubuhi watapata fursa ya kuaga mwili hadi saa 6 mchana. Saa 8 mchana, siku hiyo mazishi yatafanyika. Ni saa 8 ili wale wanaoguswa na kutamani kushiriki wasafiri

Ukitoka Dar unaweza kufika Mtwara kabla ya saa 8, ukazika na kuwahi kurudi - Wakaosafiri kwa ndege, tutatumia viwanja vya Mtwara na Nachingwea. Mwili utatua Nachingwea. Nachingwea na Masasi ni Km 35 ni jirani kuliko uliko Uwanja wa Mtwara

Updates
KUFUATIA KIFO CHA MKAPA: BENDERA ZA KENYA KUPEPEA NUSU MLINGOTI

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametangaza siku 3 za maombolezo ya Kitaifa nchini humo na bendera zitapepea nusu mlingoti kuanzia Julai 27 - Julai 29 kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa

Amesema, "Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Bendera ya Kenya zitapepea nusu mlingoti. Bendera ya Kenya itafanya hivyo kwenye majengo yote ya Serikali pamoja na Balozi zake"

Ameongeza kuwa hiyo ni ishara ya heshima na shukrani kwa jukumu kubwa ambalo Mkapa alichukua katika kukuza mshikamano ndani ya Taifa lao, na kwa kuzingatia heshima kubwa aliyonayo katika Taifa la Kenya

Amesema, "Kenya tutashukuru milele kwa jukumu muhimu lililochezwa na Marehemu Rais Mkapa katika mchakato wa upatanishi uliomaliza vurugu za baada ya Uchaguzi na machafuko ya kisiasa 2007/08"

Amesisitiza, "Amani ya Taifa letu, maridhiano na umoja mkubwa unaweza kuhusishwa moja kwa moja na vitendo, hekima, upatanishi na kujitolea kwa Rais na Marehemu Mkapa na wenzake"

Soma: President Uhuru Kenyatta has declared three days of national mourning with flags set to fly at half-mast in honour of late President Mkapa


Updates
KIFO CHA RAIS MKAPA: ACT WAZALENDO YAAHIRISHA SHUGHULI ZA KISIASA LEO

Kiongozi wa Chama hicho, Zitto Kabwe amesema wameahirisha shughuli ya Wananchi wa Lindi kumkaribisha Bernard Membe ili kupisha maombolezo ya kifo cha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa

Taarifa ya Kiongozi huyo imetoa pole ikisema "Tunaendelea kuwapa pole Watanzania na Famiia ya Rais Mkapa kwa msiba mzito huu. Maisha ya Mkapa kiuongozi ni Mafunzo"

Jana, Zitto alifanya ziara ya kimkakati katika Jimbo la Nachingwea Mkoani Lindi ya ukaguzi wa uhai wa chama na kuwataka Viongozi na Wanachama waendelee kujiandaa kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao


Updates
KIFO CHA MKAPA: RAIS MUSEVENI ATUMA SALAMU ZA POLE. BENDERA KUPEPEA NUSU MLINGOTI SIKU 3

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ametuma salamu za pole kwa Mama Anna Mkapa na Watanzania wote. Amesema Bendera za nchi yao zitapepea nusu mlingoti kwa siku 3 kuanzia leo

Amesema, "Nimepata taarifa ya kifo cha Kaka yetu, Benjamin Mkapa kwa masikitiko makubwa. Nilianza kufanya kazi na Mkapa mwaka 1967 tulipokuwa Chuo na alikuwa Mhariri Mkuu wa gazeti"

Ameongeza "Wakati wa mzozo wa mwaka 1979, Mkapa alipewa jukumu la kushughulikia Mkutano wa Moshi uliovileta pamoja vikundi vya Waganda waliozuiwa kuingia nchini kikiwemo FRONASA. Alikuwa Waziri wa Mambo ya nje wakati huo"

Rais Museveni amesema kuwa Mkapa alipokuwa Rais walifanya kazi pamoja kuunganisha Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuwa kifo chake ni pigo kubwa kwa Afrika

Soma: Museveni mourns Tanzania’s Mkapa


JULAI 26, 2020 - UPDATES
WAZIRI MKUU AKAGUA SEHEMU UTAKAPOWEKWA MWILI WA RAIS MKAPA ILI KUAGWA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekagua Kibanda Maalum kilichopo katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar ambapo mwili wa Marehemu Mzee Benjamin Mkapa utawekwa kwa ajili ya kuagwa

Watanzania wote watapewa fursa ya kuaga mwili wa marehemu kwa siku 3 kuanzia leo, Julai 26 hadiJulai 28, 2020 kabla ya mwili huo kupelekwa Lupaso, Mtwara kwa ajili ya mazishi

Zoezi la kuaga litaanza mara baada ya kumalizika kwa misa itakayofanywa na Kanisa Katoliki itakayoanza saa nne asubuhi hii

A2ECAFE8-356D-4644-9E09-F10956D034B5.png


5B001043-9780-4B45-BB7C-109F0FAA614E.png


Updates:
Shuhudia Msafara wa Kuuleta mwili wa Rais Mkapa Uwanja wa Uhuru.

Mwili wa Rais Mkapa unatarajiwa kuaga katika kiwanja hicho kuanzia leo. Watanzania wote watapewa fursa ya kuaga mwili wa marehemu kwa siku 3 kuanzia leo, Julai 26 hadiJulai 28, 2020 kabla ya mwili huo kupelekwa Lupaso, Mtwara kwa ajili ya mazishi

Updates:
Mwili wa Rais Mkapa umeshafika Uwanja wa Uhuru na sasa ni Ibada ya Misa takatifu ya kumuaga Marehemu. Baada ya Misa kila Mtanzania atapata fursa ya kuuaga mwili wa Marehemu.

when visiting any JamiiForums.com page, such as this one. 

No comments

Powered by Blogger.